6 Julai 2026 - 14:12
Washington post: Familia Nyingi Zilishiriki Katika Mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Iran

Gazeti la Washington Post limesema kuwa Mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Iran yalishuhudia ushiriki mkubwa wa wananchi, wakiwemo familia zilizofika na watoto wao, huku yakieleza kuwa tukio hilo lilidhihirisha mshikamano wa kitaifa na uthabiti wa wananchi.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) –ABNA– gazeti la Marekani la *Washington Post limeandika kuwa mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran yalihudhuriwa na umati mkubwa wa wananchi, wakiwemo familia nyingi zilizofika pamoja na watoto wao.
 
Kwa mujibu wa gazeti hilo, barabara zote zinazoelekea eneo la msikiti wa Musalla zilijaa maelfu ya waombolezaji. Lilibainisha kuwa mazingira ya tukio hilo yalikuwa ya maombolezo makubwa yaliyoambatana na ujumbe wa mshikamano na uthabiti wa kisiasa.
 
Ripoti hiyo ilieleza kuwa, sambamba na sauti za maombolezo na dua, waombolezaji walikuwa wakitoa kaulimbiu mbalimbali, zikiwemo za kusisitiza kuendelezwa kwa mapambano dhidi ya maadui wa taifa. Pia mabango yaliyobebwa na washiriki yalionesha ujumbe wa kusisitiza kuwa, licha ya majonzi waliyonayo, hawatayumba katika msimamo wao.
 
Washington Post pia ilibainisha kuwa familia nyingi zilihudhuria mazishi hayo zikiwa pamoja na watoto wao, huku baadhi ya akina mama wakionekana wakiwabeba watoto wachanga mikononi au wakiwasukuma kwa mikokoteni maalumu katikati ya umati wa waombolezaji.
 
Gazeti hilo lilihitimisha kwa kueleza kuwa, kwa mtazamo wake, mazishi hayo makubwa yamekuwa kipimo muhimu cha kuonesha uwezo wa Iran kudumisha mshikamano wa kitaifa na kiwango cha uungwaji mkono wa wananchi katika kipindi kinachotajwa kuwa miongoni mwa nyakati nyeti zaidi katika historia ya kisasa ya nchi hiyo.

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha